Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Q Jay ambaye aliwahi kutamba na kibao cha Sifai imeelezwa kuwa kwa sasa hali yake kiakili haipo sawa.
Akiongea na Bongo5 rafiki wa karibu na msanii huyo, Makamua amesema kuwa kwa sasa Q Jay yupo Bukoba na kwasasa amekuwa kama chokaraa kwani amekuwa anaokota makopo na kuongea vitu visivyoeleweka.
Akielezea chanzo hasa cha tatizo hilo, Makamua amesema kuwa ni kutokana na ugumu wa maisha pia na msongo wa mawazo kutokana na kuachana na familia yake.

